Tuesday, May 21, 2013

Wakazi wa Tanga sasa kulipia maji kupitia Vodacom M-Pesa na Airtel Money


  Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya maji safi Mkoa wa Tanga,(UWASA) Injinia Joshua Mgenyekwa(katikati) akimshuhudia Mkuu wa kitengo cha biashara cha M-pesa Vodacom Tanzania,Bw.Jackson Kiswaga kushoto akisaini mkataba kwa ajili ya kutoa huduma ya M-pesa kwa wakazi wa mkoa wa Tanga,ambapo watakuwa wakilipia Ankara za maji kwa mara ya kwanza  kupitia huduma hiyo na Airtel Money,kulia ni Meneja wa kanda ya kaskazini wa Airtel Bw.Stephen Kimea.
 Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya maji safi(UWASA) Mkoa wa Tanga,Injinia Joshua Mgenyekwa(katikati) akibadilishana nyaraka walizosainiana zinazohusu makubaliano ya kutoa huduma ya M-PESA na Mkuu wa kitengo cha biashara cha M-pesa Vodacom Tanzania,Bw.Jackson Kiswaga.Ambapo wakazi wa mkoa huo watakuwa wakilipia Ankara za maji kwa mara ya kwanza  kupitia huduma hiyo na Airtel Money,kulia ni Meneja wa kanda ya kaskazini wa Airtel Bw.Stephen Kimea.
  Baadhi ya wafanyakazi wa taasisi ya maji safi Mkoa wa Tanga,(UWASA)wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania na Airtel,mara baada ya kusainiana mkataba wa kampuni hizo mbili kutoa huduma ya malipo ya Ankara za maji kupitia huduma ya M-PESA NA Airtel Money.
---
 Tanga, Zaidi ya wananchi 700,000 waishio katika manispaa ya Tanga sasa hawatahitaji tena kupanga foleni ili kulipia ankara za maji. Hii inafuatia ushirikiano baina ya Vodacom Tanzania na mamlaka ya maji safi na maji taka ya Tanga (UWASA)  utakaowezesha malipo hayo kufanyika kupitia huduma ya M-Pesa na Airtel Money.

(UWASA) ni mamlaka iliyoundwa kisheria chini ya sheria ya utoaji maji kifungu cha 272 ili kuendesha shughuli za upatikanaji wa maji safi na kusimamia maji taka mjini Tanga.(UWASA) ilianza kufanya kazi zake kama taasisi huru mwezi Januari, 1998

Huduma ya M-Pesa ina mawakala zaidi ya 40,000 nchi nzima, hivyo kuwezesha urahisi wa malipo ya huduma ya maji kama hii mahala popote pale nchini.

Katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa UWASA,Injinia Joshua Mgenyekwa, alizungumzia jinsi ambavyo kwa kiwango kikubwa wakazi wa Tanga wataepuka usumbufu wa kutumia muda mrefu kwenye foleni za kulipia huduma ya maji na kusema: "Huduma hizi ni hatua ya kipekee hasa ikizingatiwa kuwa kuanzia sasa muda ambao mteja angeutumia kusubiri kwenye foleni, badala yake atauingiza katika shughuli nyingine za kila siku kama kazi au biashara. Pia kufanya malipo kupitia M-Pesa au Airtel Money kutarahisisha ufanyaji kazi wa mamlaka na kutoa nafasi ya kuongeza ubora wa huduma."

Mkuu wa kitengo cha biashara cha M-pesa Vodacom Tanzania,Bw.Jackson Kiswaga alisema: "Nawahimiza wakazi wa Tanga watumie huduma ya M-Pesa kulipia ankara za maji kutokana na kuwa ni huduma ya haraka na salama. Hii ni njia ya uhakika ya kuokoa muda malighafi muhimu wa muda, na hivyo ni vyema sote kuitumia."

Edward Hoseah: Tunaweza kukomesha rushwa Tanzania


Mhojiano yalifanywa na Deodatus Balile, Dar es Salaam
Edward Hoseah, mpambanaji wa juu kabisa wa Tanzania dhidi ya rushwa katika viwango vyote vya serikali, anasema nchi inaweza kujinasua na athari za ubovu wa rushwa na kuwa moja ya nchi zenye rushwa ndogo kabisa duniani.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Edward Hoseah akizungumza na mashirika ya asasi za kijamii juu ya mafanikio ya taasisi hiyo hadi sasa katika Hoteli ya Mövenpick jijini Dar es Salaam mwezi Machi 2012. [Na Deodatus Balile/Sabahi]
Hoseah anaongoza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) nchini na pia ni mwenyekiti wa Bodi ya Umoja wa Afirika (AU) ya Kupambana na Rushwa.
Tangu alipochukua nafasi ya mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU mwaka 2006, taasisi hiyo imesaidia sana kupunguza rushwa na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika orodha ya rushwa duniani kote, Hosea anaiambia Sabahi katika mahojiano.
Lakini licha ya mafanikio hayo, Hosea anasema kuwa taasisi yake inahitaji na kupewa mamlaka zaidi ili kuwa ya mafanikio zaidi, ikiwa ni pamoja na nguvu za kushitaki.
Sabahi: Ziko wapi kazi kuu zilizokabidhiwa TAKUKURU?
Edward Hoseah: Wajibu wetu mkuu ni kuzuia rushwa nchini. Tunaishughulikia rushwa kutoka pande tatu. Kwanza ni kuzuia, ambako kunajumuisha usimamiaji wa kiwango [kikubwa] cha uhawilishaji fedha na kuchunguza mienendo ya kisasa [juu ya vipi watu wanabadilishana fedha].

HEBU CHEKI JINSI MHE.TUNDU LISSU NA ANNE KILANGO VIDOLE NA MACHO YAO..!


Baada ya Bunge kuahirishwa jana, nje ya ukumbi hali haikuwa nzuri baina ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela.
Mtafaruku huo uliibuka baada ya Kilango kusikika akimtuhumu Lissu kwa uchochezi, akisema kwamba amekuwa mbunge pekee anayeongoza kwa vurugu.
  
Maneno hayo hayakumfurahisha Lissu ambaye alishindwa kuvumilia na kumgeukia Kilango kwa nguvu huku baadhi ya wabunge wakishuhudia na wengine wakimzuia Lissu.Chanzo:differentsource.com

Kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa:Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe azungumza na Mabalozi kuhusu Mkutano ujao wa Smart Partnership



Meneja wa Maandalizi ya Mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano ya Manufaa kwa Wote (Smart Partnership Global Dialogue 2013), Bibi Rosemary Jairo akiwaeleza Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa (hawapo pichani) hatua zilizofikiwa katika kuandaa mkutano huo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) akizungumza na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa yaliyopo hapa nchini (hawapo pichani) kuhusu Mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote (Smart Partnership Global Dialogue 2013) utakaofanyika Jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 28 Juni hadi 01 Julai 2013. Mkutano huo ambao utahudhuriwa na Marais mbalimbali na Wajumbe zaidi ya 500 kutoka ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unalenga  kuwanufaisha Watanzania kiuchumi, kiteknolojia na kijamii. Wengine katika picha ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (kushoto) na Mkuu wa Mabalozi ambaye pia ni Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hapa nchini, Mhe. Juma  Khalfan Mpango.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha (kushoto, mstari wa kwanza) na Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Maharage pamoja na baadhi ya Mabalozi wakimsiliza Mhe. Membe (hayupo pichani).
Mabalozi wengine wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)
Baadhi ya Mabalozi wakisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Bibi Jairo (hayupo pichani) kuhusu maandalizi ya mkutano huo.

Baadhi ya Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozungumza nao kuhusu Mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano ya Manufaa kwa Wote (Smart Partnership Global Dialogue 2013)

Picha zaidi za baadhi ya Mabalozi waliohudhuria Mkutano huo.
Mkuu wa Sekrtarieti ya Maandalizi ya Mkutano huo hapa nchini, Bibi Victoria Mwakasege (kushoto) akiwa  na Bibi Jairo wakati wa mkutano wa Mhe. Membe na Mabalozi.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki akiwa na Bw. Japhet Mwaisupule, Afisa Mambo ya Nje Mkuu wakati wa mkutano kati ya Mhe. Membe na Mabalozi.

Baadhi ya Mabalozi wakisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Bibi Jairo (hayupo pichani) kuhusu maandalizi ya mkutano huo.
Picha zaidi za mkutano kati ya Waziri Membe, Mabalozi na Wakuu wa Masharika ya Kimataita waliopo hapa nchini

Mhe. Membe akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu mazungumzo yake na Mabalozi. Wengine katika picha ni Mkuu wa Sekretarieti ya Maandalizi ya Mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano kwa Manufaa ya Wote, Bibi Mwakasege (kulia) na Meneja wa Maandalizi ya Mkutano huo Bibi Jairo (kushoto).Picha Zote na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

RAIS KIKWETE AMWAGIA SIFA LOWASSA......AMEDAI KWAMBA LOWASSA NI "JEMBE"


Rais Jakaya Kikwete amemwagia sifa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa hatua ambayo inaweza kutafsiri mengi katika medani ya siasa nchini.
 
 Akizungumza na wabunge wa CCM kwenye Ukumbi wa White House Dodoma juzi, Rais Kikwete ambaye pia mwenyekiti wa chama hicho, alisema nguvu za Lowassa pekee zinatosha kushinda uchaguzi mdogo wa kiti cha udiwani Kata ya Makuyuni kilichoko wilayani Monduli.

Kata ya Makuyuni iko wilayani Monduli, ambako Lowassa amekuwa mbunge wake tangu mwaka 1995.

Habari za kutoka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa Rais Kikwete alitoa kauli hiyo kuhusu kampeni za uchaguzi huo wa Makuyuni, baada ya kuwa ametoa ruksa kwa makada wa chama hicho wanaotaka urais kuanza kujipitisha pitisha miongoni mwa wanachama wa chama hicho. 


Lowassa anatajwa kuwa miongoni mwa wanaCCM wanaotaka kumrithi Rais Kikwete kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

“Sina tatizo na pale Makuyuni, najua muscles (misuli) za Mzee Lowassa zinatosha kutupa ushindi; au vipi mzee?” alidokeza mmoja wa wabunge wa CCM akimnukuu Rais Kikwete.

Uchaguzi wa Udiwani Kata ya Makuyuni unaotarajiwa kufanyika Juni 16, mwaka huu, utakuwa wa ushindani mkali kati ya CCM na Chadema ambao historia yao kisiasa mkoani Arusha ni ya uhasama.

Katika uchaguzi huo, unaofanyika baada ya kifo cha Abdillah Warsama (CCM), chama hicho kitatetea nafasi yake kwa kumsimamisha Godluck Lerunya na Chadema ni Japhet Sironga. 


Mbali na Kata ya Makuyuni, uchaguzi wa udiwani mkoani Arusha utafanyika pia katika Kata za Kaloleni, Themi, Kimandolu na Elerai, kutokana na waliokuwa madiwani wa kata hizo (Chadema), kufukuzwa na chama chao.

“Mnaweza kuchafuana leo, kesho mkapata mgombea mwenye nundu nyingi na mabandeji kila mahala, halafu mkapata shida kumnadi,” alisema.

 
Siyo mara ya kwanza kwa Kikwete kumsifia Lowassa kwani aliwahi kufanya hivyo mwaka jana huko Longido wakati akikabidhi ng’ombe.
 

Pia aliwahi kumsifia wakati wa kampeni za uchaguzi za mwaka 2010 wakati Kikwete alipomwelezea Lowassa kama Mbunge makini na kuwaomba watu wa Monduli kumchagua tena.

Hata hivyo, alipoulizwa kama baada ya kuruhusiwa kuanza kujipitisha kwa wanaCCM kama anataka kuwania urais, Lowassa alijibu kupitia watu wake wa karibuni kuwa asingependa kuzungumzia suala hilo hasa baada ya Rais kutoa kauli hiyo.

Kutangaza nia ruksa

Rais Kikwete aliwaeleza wabunge hao kuwa si kosa kwa watu kutangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ikiwamo urais mwaka 2015.


“Wabunge na mawaziri wenye nia ya kutangaza nia ya kugombea urais wawe huru, kwani hiyo ni haki yao, isipokuwa wafanye kwa wema bila kukivuruga chama na kuwagawa wanaCCM katika makundi. Sioni tatizo watu kujipitisha. Sisi sote hapa tulijipitisha. Lakini tufanye hivyo kistaarabu bila kuvurugana.”'

Aliwaagiza wabunge wa chama hicho kwenda majimboni mwao kusikiliza kero za wananchi badala ya kusubiri wakati wa uchaguzi.

Kauli ya Membe

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ambaye naye anatajwa kuwa miongoni mwa wagombea amewataka waandishi waache kuandika kila siku habari za urais na badala yake waandike mambo ya maendeleo. 



Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kukutana na mabalozi wa nchi zinazoendelea kuhusu Mkutano wa Smart Partnership, unaotarajiwa kufanyika nchini, Membe alisema ni vizuri yakaandikwa mambo ya maendeleo na si kila wakati kuandika mambo ya urais.

“Mkutano kama huu nchi kama Kenya watauripoti vizuri na kwa undani hivyo mfanye hivyo si kila kitu urais 2015,” alisema Membe.


 Mkutano huo utaanza Mei 28, hadi Juni Mosi na utajadili jinsi gani sayansi na teknolojia vinaweza kutumika kuzikwamua kiuchumi.

CHANZO: MWANANCHI

Chosha Maadui, Wema Sepetu Apata Mkataba Mkubwa Awa Staa Mwenye Thamani Kubwa kuliko Wanawake wote Tanzania

Miss Tanzania 2006 na muigizaji wa filamu Wema Sepetu amepata mchongo wenye pesa ndefu kutoka kampuni ya nywele ya Darling Hair Tanzania.
Kwa mujibu wa meneja wake, Martin Kadinda mkataba huo utamfanya
Wema awe staa mwenye thamani kubwa zaidi Tanzania ingawa amesema si kawaida yao kutaja kiasi cha fedha.
Deal hiyo itamuonesha Wema akiwa kama msemaji na sura wa Darling Hair Tanzania
CHANZO DJ SEK BLOG

Monday, May 20, 2013

TASWIRA KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS:MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHANI MSIBA WA ALLY SYKES JIJINI DAR


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiaga na Mzee, Harith Mwapachu na kulia ni Balozi. Paul Rupia wakati  wakati alipokuwa akiondoka baada ya kuhani msiba wa mwasisi wa TANU, Ally Sykes, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa kuzikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji mjane wa marehemu Ally Sykes, Zainab Ally, wakati alipofika kuhani msiba huo wa mwasisi wa TANU, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa marehemu Ally Sykes, wakati alipofika kuhani msiba huo wa mwasisi wa TANU, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu katibu mkuu wa CHADEMA Taifa, Zitto Kabwe Afunika Tabora


Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu katibu mkuu wa CHADEMA taifa, Zitto Zuberi Kabwe akiunguruma mbele ya mamia ya wanachama wa Chadema Mjini Tabora Jana Wakati wa Uzinduzi wa matawi ya chama katika kila Kata ya Mji huo.

Wakati huo huo chadema kimefanya ufunguzi wa kampeni za uchaguzi wa vijiji katika jimbo la Naibu Katibu Mkuu wa CCM  mwigulu nchemba Zilifunguliwa na Ally Bananga .Uchaguzi ni wa Vijiji 8 na Vitongoji 28.Picha na Habari na Chadema

KILICHOMPATA MADAM RITA KINASIKITISHA!





Na Imelda Mtema
KILICHOMPATA Madam Rita kinasikitisha! Ndivyo unavyoweza kusema ukibahatika kumuona the big boss wa Benchmark Production inayoratibu Shindano la Bongo Star Search, Rita Poulsen ‘Madam’ anayetembelea magongo baada ya kupata ajali mbaya ya gari.
Rita Poulsen ‘Madam’.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda baada ya kuwa kimya muda mrefu ikielezwa kuwa alipata ajali hiyo kitambo, Madam Rita alisema kuwa kwanza kabisa anamshukuru Mungu kwani anaamini kila kitu kinachotokea chini ya jua kina sababu yake na hata alipopata ajali hiyo alimshukuru kwa kutoka salama.
Madam Rita aliendelea kueleza kuwa ajali hiyo aliipata katikati ya Jiji la Dar  na kusababisha kuvunjika kwa kifundo ‘enka’ cha mguu wa kulia hivyo kumsababishia kutembelea magongo baada ya hospitali kumuwekea ‘hogo’.
“Namshukuru Mungu kwanza kwa kunitoa salama katika ile ajali japokuwa sijapona vizuri,” alisema Madam Rita.
Mkurugenzi huyo aliendelea kueleza kuwa alipopata ajali hiyo alikimbizwa katika Hospitali ya Muhimbili kwenye Taasisi ya Mifupa ya Moi lakini hali ilipokuwa kuwa mbaya alihamia katika hospitali moja ya Kichina ambapo kwa sasa amepata nafuu.Chanzo:www.globalpublishers.info

TANZANIA DAIMA: MAWAZIRI WATATU KUNG'OLEWA

DSC 0030 bf0b6Pia unaweza kubonyeza...http://Wwwmasterkif.blogspot.com

TUMEMUUA DK. MASSAU


Na Mwandishi Wetu
JIJI la Dar es Salaam bado linazizima kufuatia kifo cha aliyekuwa mwasisi wa Taasisi ya Moyo Tanzania (THI), Dk. Ferdinand Massau Magessa aliyefariki dunia, majira ya saa 12 jioni ya Mei 16, mwaka huu katika Hospitali ya Aga Khan, Dar, Ijumaa Wikienda lina mkasa wa kukutoa machozi.
Jeneza lenye mwili wa Dk. Massau.
Kwa mujibu wa msemaji wa familia, Cosmas Mkama, Dk. Massau aliyekuwa bingwa wa magonjwa ya moyo, alifariki dunia baada ya kusumbuliwa na kidonda kwenye koo sanjari na malaria.
“Kwa muda mrefu marahemu alikuwa akisumbuliwa na kidonda kwenye koo hali iliyomfanya awe anakula kwa kutumia mrija kwa sababu alikuwa akisikia maumivu wakati wa kumeza.
“Mbaya zaidi akiwa bado anasumbuliwa na tatizo hilo akapatwa malaria, tukampeleka Aga Khan ambako alifariki dunia,” alisema Mkama akiwa kwenye msiba nyumbani kwa marehemu, Mbweni Kwajumbe, jijini Dar.
Mwili wa marehemu uliagwa jana saa 5:00 asubuhi katika Hospitali ya Aga Khan na kusafirishwa leo kwenda Kijiji cha Murutunguru, Ukerewe, Mwanza kwa mazishi huku kifo chake kikiibua mengi.
Dk. Massau na mkewe siku ya harusi yao.
KWA NINI ‘TUMEMUUA’?
YESU alitumwa na Mungu kwenda Israel kuwaambia Wayahudi neno lake ambalo linaokoa lakini watu hao walimkataa na kumuua, ndivyo inavyoweza kutafsiriwa kwa marehemu Dk. Massau aliyekuwa shujaa mzalendo.
Kwamba, kufuatia kuongezeka kwa magonjwa ya moyo nchini, aliamua kuacha kazi ya ‘mapesa mengi’ nchini Marekani ambako alilipwa mshahara mnono na kuleta ukombozi Tanzania kwa kufungua hospitali ya kutibu magonjwa ya moyo, lakini serikali ilionekana kumkataa.
Serikali ni kama ilimkataa kufuatia kitendo cha Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF kumnyang’anya jengo walilompangishia kufanyia kazi na kuwaondoa wagonjwa waliokuwa wamelazwa kwa madai ya kumdai kodi bila kujali kuwa alikuwa akitetea roho za Watanzania wenzake wanaoteswa na magonjwa ya moyo.
Kuanzia hapo, habari zinasema hali ya afya ya daktari huyo ilianza kubadilika ambapo watu wake wa karibu wanadai ‘stress’ au mawazo yalikuwa yakimchanganya kila kukicha.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa msibani.
Ni kweli amefariki dunia kutokana na kidonda kwenye koo na malaria, lakini yapo madai kuwa kitendo alichofanyiwa na NSSF, kwake kilikuwa cha ajabu kwa vile alitegemea taasisi yake ingeungwa mkono kwa vile ilikuwa ikiwasaidia Watanzania walala hoi wasiokuwa na uwezo wa kwenda kutibiwa nchini India.
Baadhi ya waombolezaji kwenye msiba nyumbani kwa marehemu, Mbweni Kwajumbe walisema dokta huyo alileta ukombozi kwa Watanzania lakini waliotakiwa kukombolewa wenyewe walikuwa hawako tayari (kama Wayahudi).
“Inauma sana! Jamaa aliipenda nchi yake ndiyo maana aliamua kuachana na nchi ya Marekani kuja kuanzisha taasisi yake nchini, lakini cha ajabu mizengwe ilikuwa mingi, alipigwa vita, mawazo yakamjaa.
“Kama uliwahi kumwona wakati anaanzisha THI mwaka 2005 afya yake ilikuwa imara, lakini ulipoanza mgogoro wa NSSF, alikongoroka sana,” alisema Magana aliyekuwa kwenye msiba huo.
Dk. Massau enzi za uhai wake.
HISTORIA YAKE KWA UFUPI
Marehemu Dk. Massau alihitimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tawi la Muhimbili mwishoni mwa miaka ya 80. Alipata mafunzo ya upasuaji wa moyo katika Chuo Kikuu cha Hubei nchini China.
Dk. Massau aliwahi kufanya kazi nchini Marekani katika Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Texas (THI) akiwa ameongeza ujuzi kwenye Chuo Kikuu cha Texas Medical.
Mwaka 1996 aliongeza ujuzi tena kupitia kwa Profesa Denton Cooley ambaye ndiye mwanzilishi na mpasuaji mkuu  katika Taasisi ya Magonjwa ya Moyo ya Texas, Marekani.
Mke wa marehemu (kulia) akiwa na simanzi.
WAMAREKANI WAMKUBALI
Baada ya kuona utendaji wake wa kazi ni wa hali ya juu, Dk. Cooley aliiandikia barua Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akitaka kumtambua Dk. Massau na uwezo wake wa kazi.
Hata hivyo, inasemekana serikali ilikaa kimya juu ya barua hiyo. Waziri wa afya alikuwa Dk. Aron Chiduo.
Mwaka 2000, Dk. Massau alirejea rasmi nchini na kufanya kazi katika Hospitali ya TMJ ambapo pia ilimsaidia kuanzisha taasisi yake.
NSSF WALIVYOMMALIZA
Aprili 2012, NSSF kupitia amri ya Mahakama Kuu kitengo cha Ardhi, iliifunga taasisi yake na kuwahamishia wagonjwa wote kwenye hospitali nyingine kwa kile kilichodaiwa ni taasisi hiyo kushindwa kulipa shilingi bilioni saba za pango.
Hadi Dr. Massau anafikwa na umauti alikuwa akiendelea na ujenzi wa jengo la taasisi yake huko Mbweni, Dar.
Marehemu ameacha mke na watoto watano. Mungu ailaze pema peponi roho ya marehemu. Amina.Chanzo:www.globalpublishers.info

Sunday, May 19, 2013

Maelfu ya Wanachama Wa Chadema Wajitokeza Kwenye Uzinduzi Wa Kampeni Ya Udiwani Arusha


Picha juu ni Maelfu ya wananchama wa Chadema Wakiwa kwenye mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za Udiwani Arusha Jana kwa ajili ya uchaguzi wa madiwani wa kata nne; Elerai, Kaloleni, Themi na Kimandolu ambazo madiwani wake walifukuzwa uanachama na chama hicho huku kikitamba kuwa hakina uchaguzi Arusha ila CCM ndio wenye uchaguzi.
 
“Arusha CHADEMA hatuna uchaguzi, sisi tuna ushindi ila CCM ndio wana uchaguzi,” alisema Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni hizo.
Lema alitumia muda mwingi kunadi sera za CHADEMA na kuongeza kuwa madiwani waliofukuzwa ndani ya chama hicho, walipokea rushwa na katika kampeni zao kwenye kila kata, watatoa ushahidi jinsi walivyopokea rushwa.
Huku akishangiliwa na wananchi wa Arusha, Lema alimuonya Mkuu wa Mkoa wa Arusha na Mkuu wa Wilaya hiyo kujiepusha na kampeni na kutoa tahadhari kuwa wakibainika wanafanya kampeni itakuwa ni makosa makubwa kwao.Katika kampeni hizo.Picha na Habari na Chadema

Rais wa Zanzibar Dk.Shein Azinduwa Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasili katika viwanja vya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Tawi la Zanzibar, akiongozana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Dk. Salim Ahmed Salim. kwa ajili ya uzinduzi wa Chuo hicho kilioko nje kidogo ya Mji wa Zanzibar Bububu.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiweka jiwe la Msingi la Jengo la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Bububu Zanzibar, kulia Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Dk. Salim Ahmed Salim na kushoto Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif hamad.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia katika sherere za uzindizi wa Chuo cha Kumbkumbu ya Mwalimu Nyerere Bububu Zanzibar.

Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. John Magotti, akitowa historia ya Chuo hicho kwa Rais wa Zanzibar katika sherere za ufunguzi wa Jengo la Chuo hicho huko Bububu Zanzibar.

Rais wa Zanzibar ma Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akimsikiliza Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. John.Mogotti akihutubia na kutowamaelezo ya ujenzi wa jengo hilo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. Salim Ahmed Salim akizungumza katika uzinduzi huowa Jengo la Chuo hicho uliofanywa na Rais wa Zanzibar Dk. Shein.

MWENYEKITI wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya MwalimNyerere Dk. Salim Ahmed Salim, akimkabidhi zawadi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, katikati Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad,

Kwa taswira zaidi endelea kutembelea ZanziNews

Rais wa Zanzibar Dk.Shein Azinduwa Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasili katika viwanja vya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Tawi la Zanzibar, akiongozana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Dk. Salim Ahmed Salim. kwa ajili ya uzinduzi wa Chuo hicho kilioko nje kidogo ya Mji wa Zanzibar Bububu.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiweka jiwe la Msingi la Jengo la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Bububu Zanzibar, kulia Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Dk. Salim Ahmed Salim na kushoto Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif hamad.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia katika sherere za uzindizi wa Chuo cha Kumbkumbu ya Mwalimu Nyerere Bububu Zanzibar.

Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. John Magotti, akitowa historia ya Chuo hicho kwa Rais wa Zanzibar katika sherere za ufunguzi wa Jengo la Chuo hicho huko Bububu Zanzibar.

Rais wa Zanzibar ma Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akimsikiliza Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. John.Mogotti akihutubia na kutowamaelezo ya ujenzi wa jengo hilo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. Salim Ahmed Salim akizungumza katika uzinduzi huowa Jengo la Chuo hicho uliofanywa na Rais wa Zanzibar Dk. Shein.

MWENYEKITI wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya MwalimNyerere Dk. Salim Ahmed Salim, akimkabidhi zawadi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, katikati Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad,

Kwa taswira zaidi endelea kutembelea ZanziNews

Rais wa Zanzibar Dk.Shein Azinduwa Tawi la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Zanzibar.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasili katika viwanja vya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Tawi la Zanzibar, akiongozana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Dk. Salim Ahmed Salim. kwa ajili ya uzinduzi wa Chuo hicho kilioko nje kidogo ya Mji wa Zanzibar Bububu.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiweka jiwe la Msingi la Jengo la Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Bububu Zanzibar, kulia Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Dk. Salim Ahmed Salim na kushoto Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif hamad.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia katika sherere za uzindizi wa Chuo cha Kumbkumbu ya Mwalimu Nyerere Bububu Zanzibar.

Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. John Magotti, akitowa historia ya Chuo hicho kwa Rais wa Zanzibar katika sherere za ufunguzi wa Jengo la Chuo hicho huko Bububu Zanzibar.

Rais wa Zanzibar ma Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akimsikiliza Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. John.Mogotti akihutubia na kutowamaelezo ya ujenzi wa jengo hilo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Dk. Salim Ahmed Salim akizungumza katika uzinduzi huowa Jengo la Chuo hicho uliofanywa na Rais wa Zanzibar Dk. Shein.

MWENYEKITI wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya MwalimNyerere Dk. Salim Ahmed Salim, akimkabidhi zawadi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, katikati Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad,

Kwa taswira zaidi endelea kutembelea ZanziNews