
Picha juu ni Maelfu ya wananchama wa Chadema Wakiwa kwenye mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za Udiwani Arusha Jana kwa
ajili ya uchaguzi wa madiwani wa kata nne; Elerai, Kaloleni, Themi na
Kimandolu ambazo madiwani wake walifukuzwa uanachama na chama hicho huku
kikitamba kuwa hakina uchaguzi Arusha ila CCM ndio wenye uchaguzi.
“Arusha
CHADEMA hatuna uchaguzi, sisi tuna ushindi ila CCM ndio wana uchaguzi,”
alisema Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini aliyekuwa mgeni rasmi
katika uzinduzi wa kampeni hizo.
Lema
alitumia muda mwingi kunadi sera za CHADEMA na kuongeza kuwa madiwani
waliofukuzwa ndani ya chama hicho, walipokea rushwa na katika kampeni
zao kwenye kila kata, watatoa ushahidi jinsi walivyopokea rushwa.
Huku
akishangiliwa na wananchi wa Arusha, Lema alimuonya Mkuu wa Mkoa wa
Arusha na Mkuu wa Wilaya hiyo kujiepusha na kampeni na kutoa tahadhari
kuwa wakibainika wanafanya kampeni itakuwa ni makosa makubwa kwao.Katika kampeni hizo.Picha na Habari na Chadema










































